
Pamoja na Kidiaba ambaye anafahamika sana kwa mtindo wa kusherehekea bao kwa kuruka kwa makalio, Pamphile Mihayo Kazembe pia ni mchezaji mwingine wa TP Mazembe anayewania ubunge kupitia chama cha upinzani cha PND.
Nahodha huyo wa Leopards mwenye umri wa miaka 39 amesema anaamini kuwa wachezaji wanaweza kuwa viongozi bora na kuleta mabadiliko ya maendeleo katika maeneo yao.

Kidiaba alianza kuichezea timu ya taifa mwaka 2002 na ameshiriki katika michuano 11 ya kufuzu katika michuano ya kombe la duniani na kwa ujumla kuichezea timu ya taifa mara 59.

0 maoni:
Chapisha Maoni