.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Alhamisi, 4 Juni 2015

Tagged Under:

Baada ya ajali ya lori la mafuta Nigeria, hii nyingine ni kituo cha mafuta kuwaka moto Ghana

By: Unknown On: Alhamisi, Juni 04, 2015
  • Share The Gag

  • mooo
    Mapema wiki hii millardayo.com iliandika stori ya ajali ya lori la mafuta kuua zaidi ya watu 90 Nigeria ikiwa ni baada ya kuwa kwenye mwendo mkali na kugonga watu na magari yaliyokuwa kwenye kituo cha abiria.
    station
    Muonekano wa kituo cha mafuta baada ya kulipuka
    Lakini leo Ghana nayo imeingia kwenye headlines baada ya kituo cha mafuta kulipuka na kuua watu wanaokadiriwa kuzidi 90 katika mji mkuu wa nchi hiyo Accra.
    Mlipuko huo umetokea baada ya mvua kubwa iliyosababisha mafuriko katika maeneo mengi ya mji huo ambapo pia imewaacha watu wengi bila makazi huku sehemu kubwa ya mji ikiwa gizani kutokana na kukatika kwa umeme.
    mtoto
    Mwili wa mtoto ukiokotwa katika eneo la kituo hicho
    Idadi ya watu waliofariki huenda ikaongezeka kwani watu wengi wamepoteza maisha baada ya kuwepo kituoni hapo wakijikinga na mafuriko yaliyotokea na huenda idadi ikaongezeka kutokana na baadhi ya miili kuwa bado haijapatikana.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni