


Mechi nyingine ya Jumanne Usiku itachezwa huko Jiji la Turin Nchini Italy wakati Wenyeji Juventus watakapoivaa AS Monaco ya France.

Real watatinga kwa maadui zao Vicente Calderon wakiwa na Kikosi kamili kwa mara ya kwanza katika Miezi Mitano.
James Rodriguez na Toni Kroos, ambao waliikosa Mechi ya La Liga ya Jumamosi walipoifunga Eibar 3-0 baada ya kuwa Kifungoni, wanarejea dimbani.

Jumatano pia zipo mechi mbili nyingine za Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI kati ya PSG na Barcelona huko Mjini Paris na nyingine itachezwa huko Ureno kati ya FC Porto na Bayern Munich.

Robo Fainali-Mechi za Kwanza
Jumanne Aprili 14
Atlético Madrid vs Real Madrid
Refa: Milorad Mažić (Serbia)
Uwanja: Estadio Vicente Calderón, Madrid, Spain
Juventus vs AS Monaco
Refa: Pavel Královec (Czech Republic)
Uwanja: Juventus Stadium, Turin, Italy
Jumatano Aprili 15
Paris Saint-Germain vs Barcelona
Uwanja: Parc des Princes, Paris, France
FC Porto vs Bayern Munich
Uwanja: Estádio do Dragão, Porto, Portugal

Fernando Torres akiwa na wenzake kwenye mazoezi huko Vicente Calderon wakijiandaa na kipute cha UEFA leo Jumanne Usiku.

Fundi...! Meneja Diego Simeone nae kwenye mazoezi

Simeone akiteta na Vijana wake wakati wa Mazoezi leo wakijiandaa vyema kuwakabili ndugu zao Real Madrid leo Jumanne kwenye UEFA.

Diego Godin, Arda Turan, Cristian Ansaldi, Antoine Griezmann na Torres wamejumuika leo kwenye zoezi

Simeone na Vijana wake hawajapoteza kwao Atletico Madrid kwenye mitanange sita tangu 2014 Champions League na leo wanaangalia kubaki na pointi


Tiago na Godin nao kwenye mazoezi.
0 maoni:
Chapisha Maoni