
BAO pekee la Christian Benteke limewapa Liverpool ushindi wa Bao 1-0 walipocheza huko Stadium of Light na Sunderland katika Mechi ya mwisho kabisa ya Ligi Kuu England.
Bao hilo lilipatikana Dakika 1 tu baada ya Kipindi cha Pili kuanza kwa Nathanial Clyne kupenyeza Mpira mbele na Adam Lallana kuugusa tu na kumkuta Christian Benteke aliefunga na kuipa Bao Liverpool.




0 maoni:
Chapisha Maoni