
Manchester City ilikuwa imeweka dau la pauni milioni £40 lakini ombi lao likakataliwa na Liverpool.
Mlinzi wa Manchester United, Luke Shaw ameorodheshwa katika nafasi ya 9, John Stones wa Everton ameorodheshwa wa 16 huku kiungo wa Arsenal Calum Chambers akiorodheshwa katika nafasi ya 19.

Inatumia vipengee kama umri,nafasi wanayocheza uwanjani,Klabu,urefu wa Kandarasi,mechi walizochezea timu zao za taifa,mechi walizocheza,mabao waliofunga,majeraha na ubora wao kitalanta.

''Hivyo vyote ndivyo vilitusaidia kubaini kuwa Sterling ndiye mchezaji bora na mwenye thamani ya juu zaidi barani ulaya kwa sasa.'' alisema bwana Esteve Calzada
Mlinzi wa Paris St-Germain ya Ufaransa ambaye ni raia wa Brazil Marquinhos ameorodheshwa katika nafasi ya pili na thamani ya pauni milioni £27.8.
Mchezaji mpya wa Manchester United vilevile ye Uingereza Memphis Depay aliyegharimu kitita cha pauni milioni £31 ameorodheshwa katika nafasi ya tatu akiwa na thamani ya pauni milioni £23.8.

Wachezaji 4 katika orodha hiyo ni raia wa Uingereza huku 9 kati ya 20 bora wakitarajiwa kucheza katika ligi kuu ya Uingereza msimu ujao.
RAHEEM STERLING AKILINGANISHWA NA WENGINE HAPA!
1. Raheem Sterling (Liverpool) £35m | 7. Mateo Kovacic (Inter Milan) £18.5m |
2. Marquinhos (Paris St-Germain) £27.8m | 8. Jose Gaya (Valencia) £18.3m |
3. Memphis Depay (Manchester United) £23.8m | 9. Luke Shaw (Manchester United) £18m |
4. Domenico Berardi (Sassuolo) £21.6m | 10. Aymeric Laporte (Athletic Bilbao) £17m |
5. Jose Gimenez (Atletico Madrid) £21.4m | 16. John Stones (Everton) £12m |
6. Hakan Calhanoglu (Bayer Leverkusen) £19.4m | 19. Calum Chambers (Arsenal) £10.6m |
0 maoni:
Chapisha Maoni