
Profesa Jiri Dvorak, Daktari Mkuu wa FIFA, ametamka kuwa Mameneja hawana haki yeyote kuwaambia Matabibu wao waingie Uwanjani au la kumtibu Mchezaji alieumia kwani jukumu hilo ni la Dokta aliepo Uwanjani.

Kitendo hicho kilimkera Mourinho kwani Mchezaji akihudumiwa na Madokta basi huwajibika kutoka nje ya Uwanja na husubiri amri ya Refa kuingia tena huku Gemu ikiendelea na hilo liliiacha Chelsea iwe Mtu 9 kwa Dakika kadhaa.

Kisha zikaibuka ripoti kuwa Mourinho ameamua kumzuia Dokta Carneiro kuhudhuria Mechi na Mazoezi ya Timu ya Kwanza ya Chelsea.
Jambo hilo limezua mjadala mkubwa huko England na wengi kumponda Mourinho.
Leo, Profesa Dvorak amesema Meneja hana wajibu wowote Mchezaji akiumia: “Kitaaluma, kitabibu, Meneja hana sauti. Hiyo ndio Sheria yetu Kitaaluma, na wajibu wetu kimaadili, kumwangalia Mchezaji tu.”
Profesa Dvorak pia ametamka Daktari ni lazima awe Benchi na anaruhusiwa kuingia Uwanjani hata bila ya ridhaa ya Refa kama akiona Mchezaji amekumbwa na tatizo la moyo au ameumia kichwani au amepoteza fahamu.
Profesa Dvorak amenena: “Hapo ni uamuzi wake Dokta na FIFA Siku zote itamuunga mkono.”
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni