Wenyeji Chile wametwaa Taji lao la
kwanza kabisa baada ya kuibwaga Argentina kwa Penati 4-1 kufuatia Sare
ya 0-0 katika Dakika 120 za Fainali ya Copa America, Kombe la Mataifa ya
Marekani ya Kusini, iliyochezwa mbele ya Halaiki ya Mashabiki ndani ya
Estadio Nacional Santiago Jijini Santiago.
Kipigo hiki kimeendeleza ukame wa
Argentina wa Miaka 22 wa kutotwaa Taji lolote tangu walipobeba Copa
America Mwaka 1993 huko Ecuador na pia unamfanya Kepteni wao Lionel
Messi, aliewahi kuwa Mchezaji Bora Duniani mara 4, aendelee kutokuwa na
mafanikio yeyote na Le Albiceleste tofauti na akiwa na Klabu yake FC
Barcelona ya Spain.
Kwa Chile, ushindi huu umemaliza Karne
yao ya kushiriki Mashindano bila Taji lolote baada ya kufanikiwa kufika
Fainali 4 za Copa America, zile za 1955, 1956, 1979 na 1987, na kufungwa
zote.
Chile,
chini ya Kocha toka Argentina Jorge Sampaoli, hawakucheza Soka la
kuvutia na walikosa nafasi moja ya wazi katika Dakika za Nyongeza 30
wakati Argentina, chini ya Kocha Gerardo 'Tata' Martino, nao walikosa
nafasi ya wazi wakati Gonzalo Higuain alipokosa ndani ya Dakika 90.
Ushindi! 4-1 kwa mikwaju ya penati

Balaa!! Alexis Sanchez alipowafungia mkwaju wa Ushindi

Alexis Sanchez akishangilia baada ya kuitoa Argentina

Mikwaju ya penati ikiendelea..


Kipa wa Chile Claudio bravo akiwa amebeba juu zawadi yake ya Golden Grove

Eduardo Vargas akiwa na mwanae pamoja na Tuzo yake

Ni shida!! Lionel Messi akiwa hoi kwa mara nyingi akichemsha ndani ya Fainali! Ukame waendelea...

Choka mbaya!

Shangwe kwa kwenda mbele huku ikiwa ni kwa mara ya kwanza kwa wenyeji Chile


Baadhi ya Wachezaji wa Chile wakipeta baada ya kushinda kwa mikwaju ya penati dhidi ya Argentina.

Argentina
wameshindwa kutamba mbele ya Chile kwenye mchezo wa Fainali wa Copa
America na kufungwa kwa mikwaju ya penati 4-1 baada ya kutoshana nguvu
dakika 120 kwa kutoka 0-0.

TASWIRA

Dakika 120 zilimalizika bila kufungana tena kwa kutoka 0-0 na mikwaju ya penati kupigwa!

Dakika 90 zilimalizika bila kufungana na kuongezwa muda wa dakika 30!

Angel Di Maria akubali yaishe mapema kipindi cha kwanza! Lavezzi alichukuwa nafasi yake

Kipindi cha pili kinaendelea..

Mashabiki wenyeji chile!
VIKOSI:
Argentina Wanaoanza: Romero, Zabaleta, Demichelis, Otamendi, Rojo, Biglia, Mascherano, Pastore, Messi, Aguero, Di Maria
Chile wanaoanza: Bravo, Isla, Medel, Silva, Beausejour, Aranguiz, Diaz, Vidal, Valdivia, Sanchez, Vargas
Chile vs Argentina, Estadio Nacional, Santiago

Mashabiki

Ni Patashika Fainali Usiku huu Copa America kati ya Chile v Argentina

Chile

Lionel Messi kufanya kazi ya ziada punde!
0 maoni:
Chapisha Maoni