
Cech, mwenye Miaka 33, ameshaafikiana maslahi yake binafsi na Arsenal na kilichobaki ni kusawazisha mvutano kati ya Chelsea na Arsenal kuhusu Ada ya Uhamisho huku pande hizo mbili zikikubaliana kuendelea na mazungumzo.
Cech amebakiza Mwaka mmoja katika Mkataba wake na Chelsea na ameruhusiwa rasmi na Mmiliki wa Klabu hiyo, Roman Abramovich, kuhamia Klabu yeyote anayotaka baada ya kusugua Benchi Msimu uliopita akiwa Kipa Namba mbili nyuma ya Thibaut Courtois.

Lakini Karata ya Trufu ya Mmiliki Roman Abramovich ndiyo imemtoa kapa Jose Mourinho na kumpa mtaji Kipa Mkongwe Petr Cech.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni