RATIBA UEFA CHAMPIONS LEAGUE:

KESHO Jumanne Usiku zipo Mechi mbili moja ikiwa huko Etihad Jijini Manchester wakati Manchester City watakapoivaa FC Barcelona na nyingine huko Mjini Turin Nchini Italy wakati Mabingwa wa Italy na Timu inayoongoza Serie A, Juventus watakapocheza na BVB Borussia Dortmund.


Katika Mechi hizo, Barcelona walishinda Mechi ya Kwanza iliyochezwa Etihad Bao 2-0 kwa Bao za Lionel Messi, la Penati, na jingine la Daniel Alves huku Martín Demichelis wa City akipewa Kadi Nyekundu.
Kwenye Marudiano huko Nou Camp, Barca ilishinda Bao 2-1 Wafungaji wao wakiwa wale wale, Lionell Messi na Alves, huku Pablo Zabaleta wa City akipewa Kadi Nyekundu.
Lakini safari hii, Meneja wa Man City, Manuel Pellegrini, anaamini City ipo kwenye hali njema zaidi kupita Msimu uliopita.
Wakati Jumamosi City ikiitwanga Newcastle United Bao 5-0 kwenye Ligi Kuu England, Barcelona ilichapwa 1-0 na Malaga kwenye Mechi ya La Liga iliyochezwa Nyumbani kwa Barca huko Nou Camp.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE
RATIBA - JUMATANO
Jumanne 24 Februari 2015
Juventus FC vs BV Borussia Dortmund
Manchester City vs FC Barcelona .
Jumatano 25 Februari 2015
Arsenal FC vs AS Monaco FC Bayer 04
Leverkusen vs Atletico de Madrid.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni