
Jana, Arsenal iliichapa Bournemouth 2-0 na kutwaa uongozi wa Ligi wakiwa na Pointi 39 kwa Mechi 19 wakifuata Leicester wenye Pointi 38 kwa Mechi 18, Tottenham ni wa 3 na wana Pointi 35 kwa Mechi 19 na wa 4 ni Man City wenye Pointi 35 kwa Mechi 18.
Leo huko King Power Stadium, Leicester wanacheza na Man City na wakishinda watarudi kileleni na wakitoka Sare watabaki Nafasi ya Pili.
Leicester wanatinga kwenye Mechi hii wakitoka kufungwa 1-0 na Liverpool na kupoteza wimbi lao la kutofungwa katika Mechi 10 wakati City ikiichapa Sunderland 4-1.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni