
Baada ya kuanza Hovyo kwa kufungwa Mechi 3, Sare 1 na Kushinda 1 tu na kujikuta wako Nafasi ya 17 wakiwa Pointi 11 nyuma ya Vinara Man City, Leo Chelsea walikamia ushindi na Diego Costa alihakikisha hilo baada ya kuwachokoza Mabeki wa Arsenal na kusababisha Sentahafu wao apande jazba na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.


Hadi Haftaimu, Chelsea 0 Arsenal 0.
Kipindi cha Pili Dakika ya 53, Frikiki ya Fabregas iliunganishwa kwa Kichwa na Kurt Zouma na kuwapa Chelsea Bao.
Dakika ya 79, Arsenal walibaki Mtu 9 baada ya Kiungo wao Santi Cazorla kupewa Kadi ya Njano ya Pili na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni