


Kama ilivyokuwa Msimu uliopita, Leo tena Swansea City wametoka nyuma kwa Bao 1 na kuifunga Manchester United Bao 2-1 na kuishushia kipigo chao cha kwanza kwenye Ligi Kuu England kwa Msimu huu mpya.
Hadi Mapumziko, Mechi hii iliyochezwa huko Liberty Stadium, ilikuwa 0-0.
Dakika 3 tu baada ya Kipindi cha Pili kuanza Juan Mata aliipa Man United Bao ikiwa ni zawadi kwa kuitawala Mechi hii yote.
Hadi Daki ya 60 Man United walionekana ni washindi lakini Dakika 1 baadae Mchezaji wa Kimataifa wa Ghana, Andre Ayew, akaisawazishia Swansea na Dakika 5 baadae, Mtu wao hatari, Bafetimbi Gomis akawapa Bao la Pili na la ushindi.

Kipindi cha pili dakika ya 48 juan mata aliwapachikia bao la kuongoza Man United na kufanya 1-0 dhidi ya Swansea City. Shaw alipiga krosi iliyompata Rooney kwa kuugusa na hatimae Juan Mata kuunganisha moja kwa moja ndani ya nyavu za Swansea City.



Depay akiendesha mpira.
Ligi Kuu England sasa inasimama kupisha Mechi za Kimataifa na itarejea tena Septemba 12 na Man United wapo kwao Old Trafford kupambana na Mahasimu wao wa Jadi Liverpool ambao Jana wakiwa kwao Anfield walinyukwa 3-0 na West Ham.

Swansea wanaoanza 11: Fabianski, Naughton, Fernandez, Williams, Taylor, Cork, Shelvey, Sigurdsson, Ayew, Routledge, Gomis
Akiba: Nordfeldt, Rangel, Bartley, Tabanou, Ki Sung-Yueng, Dyer, Eder
Manchester United wanaoanza 11: Romero, Darmian, Smalling, Blind, Shaw, Schneiderlin, Schweinsteiger, Mata, Herrera, Memphis, Rooney
Akiba: Johnstone, McNair, Valencia, Carrick, Young, Fellaini, Chicharito
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni