
Ba mwenye umri wa miaka 30 alikua anatarajiwa kurudi katika ligi kuu ya England, lakini ameamua kuelekea mashariki ya mbali kusakata kabumbu.
Mchezaji huyu wa zamani wa vilabu vya Newcastle na Chelsea, alifunga mabao 27 katika michezo 44 aliyoicheza timu ya Besiktas, msimu uliopita.

Baadae akatimkia Ujerumani kwa miaka 4 akiitumika klabu ya Hoffenheim msimu wa 2011 akajiunga na wagonga nyundo wa London West Ham.
Baada ya kufanya vizuri na West Ham akajiunga na Newcastle katika msimu wa 2011/12alipofunga mabao 29 katika michezo 57 kabla ya kuhamia Chelsea na kucheza michezo 51 akizifumania nyavu mara 14.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni