
James Milner wa Man City ajiunga na Liverpool.
Liverpool wameafikiana Dili ya kumsaini Kiungo wa England James Milner ambae anachezea Manchester City kwa Uhamisho wa bure.
Milner,
mwenye Miaka 29, ameshakubaliana malupulupu yake binafsi na Liverpool
na atajiunga rasmi nao kama Mchezaji Huru wakati Mkataba wake na City
utakapomalizika hapo Julai Mosi kama akifuzu upimwaji Afya yake.
Akiwa
na City kwa Miaka Mitano, Milner alifanikiwa kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu
England mara 2, FA CUP na Kombe la Ligi, Capital One Cup.
Milner pia ameichezea England mara 53.
Msimu uliopita, Milner alianza Mechi 24 na kufunga Bao 8 na kuifungia City Bao 8.
Mchezaji
huyu alijiunga na City iliyokuwa chini ya Roberto Mancini Mwaka 2010
kwa Dau la Pauni Milioni 26 akitokea Aston Villa na kuichezea Klabu hiyo
jumla ya Mechi 125 na kufunga Bao 18.
Klabu nyingine alizowahi
kuzichezea ni Newcastle United na Klabu ya Mji wa Nyumbani kwao Leeds
United ambayo alianza kucheza Ligi Kuu England kwa mara ya kwanza Mwaka
2002 akiwa na Miaka 16 tu.

Ilkay
Gundogan kujiunga na Manchester United msimu wa 2015/16? Klabu kama
Barca, AC Milan na Bayern Munich zilikuwa zikihitaji sahihi yake huku
mapema tetesi zikisema wenda akapimwa afya kujiunga na Barcelona.

Ilkay Gundogan

Christian Funchs wa Schalke atua Leicester City

Memphis Depay wa PSV - Ni wa Manchester United mpaka sasa akitokea PSV Eindhoven

Morgan
Schneiderlin kujiunga na Klabu ya Man United baada ya kushinda mbio
hizo huku Klabu ya Arsenal nayo ikiwa kwenye mchakato huo huo wa
kumwania mchezaji huyo.

Christian Atsu wa Chelsea atua kwa Mkopo Bournemouth

Philipp - Bayer Leverkusen kwenda Stoke

Xavi - Al -Sadd

Kipa Artul Borus - Southampton kwenda Bournemouth

Graham Dorrans - West Brom kwenda Norwich

Joshua King - Blackburn kwenda Bournemouth

Winger wa Benfica Nicolas Gaitan nae inasemekana kujiunga na Man United

Boyata wa Man City kwenda Celtic

Luiz Gustavo anukia Old Trafford
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni