
Kwa mujibu wa The Currant Bun, “Manchester United wanakaribia kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid, Mario Mandzukic”.
Mandzukic ameibuka kuwa mchezaji anayewaniwa zaidi na Man United ili kutengeneza muunganiko na Wayne Rooney msimu wa 2015/2016 chini ya kocha Louis van Gaal.

Mario Mandzukic ni jibu kwa Van Gaal?
Mcroatia huyo alianza kuonesha cheche akiwa Bayern Munich na msimu uliopita alicheza vizuri akiwa na Atletico Madrid, lakini wachambuzi wengi wa soka hawamuweki kwenye kundi la washambuliaji wa kiwango cha juu zaidi duniani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni