
Bondia kutoka Ufilipino, Manny Pacquiao anatarajia kufanyiwa upasuaji wa bega la mkono wa kulia, ikiwa ni siku tatu zimepita baada ya kupoteza pambano lake dhidi ya bondia Floyd Mayweather wa nchini Marekani.

Kwa mujibu wa tovuti ya ESPN bondia huyo alipambana na Mayweather huku akiwa na maumivu makali ya bega.


Taarifa nyingine zinaeleza kwamba Pacquiao, hakufanya mazoezi kwa siku kadhaa kutokana na maumivu ya bega ambayo aliyatonesha kutokana na maandalizi makali ya pambano lake dhidi ya Floyd Mayweather.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni