
Fowadi wa Valencia CF Paco Alcacer akishangilia bao lake la dakika ya 19

Wachezaji wa Valencia wakipongezana baada ya Javi Fuego kumfunga kipa wa Real Iker Casillas kwa mpira wa adhabu

Valencia walitangulia kipindi cha kwanza kwa kufunga bao 2-0

Ronaldo leo hoi!! Bernabeu

Pepe alianza kurudisha bao kipindi cha pili dakika ya 56 na Isco dakika ya 84 kusawazisha bao na kufanya 2-2 na mtanange kumalizika.
Sare hii inawafanya Real kugawana pointi moja moja na Valencia huku Barcelona wakiwazidi pointi 4 Kileleni Real ambao wako nafasi ya pili. Barca wako Kileleni wakiwa na pointi zao 90 na Real wametimiza pointi 86. Nafasi ya tatu inashikiliwa na Atletico de Madrid wenye pointi 76.
Valencia CF pamoja na kuwa mbele ya bao 2-0 dhidi ya Real na kulazimishwa sare wao wapo nafasi ya 4 na pointi zao 73.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni