
City Jumatano Usiku wapo Nou Camp kurudiana na Barcelona baada ya kuchapwa 2-1 na Barca wakiwa kwao Etihad Wiki 3 zilizopita katika Mechi ya kwanza.

Kwa hali za Timu hizi mbili hivi sasa, Barca wako vyema zaidi baada ya kupanda kileleni mwa La Liga kufuatia ushindi wao wa Mechi 16 kati ya 17 zilizopita.


Hata hivyo, Meneja wa City anaetoka Chile, Manuel Pellegrini, amesisitiza bado wana matumaini ya kuibwaga Barca kwao.
Lakini hiyo si kazi rahisi hata kidogo ukichukulia fomu ya Barca hivi sasa na ukali wa Fowadi yao ya Mtu 3 ya Lionel Messi, Neymar na Luis Suarez.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni