

Ndani ya Uwanja wa Stadio Olimpico usiku huu ilishindukana kutoa mshindi baada ya Wenyeji AS Roma kutoka Sare na Juventus ya Bao 1-1 kwenye Mechi ya Ligi Serie A.
Matokeo hayo yameifanya Juve iendelee kuongoza Ligi hiyo ya Italy ikiwa Pointi 9 mbele ya Timu ya Pili AS Roma.
Juve walifunga Bao lao kwa Frikiki ya Dakika ya 64 iliyotolewa baada ya Vasilis Torosidis kumchezea Rafu Vidal na Beki huyo wa AS Roma akapewa Kadi Nyekundu.
Licha ya kucheza Mtu 10 AS Roma walisawazisha Dakika ya 78 kwa Kichwa cha Seydou Keita alieunganisha Frikiki ambacho kilimgonga Marchisio na kutinga.
Juventus XI (3-5-2)
Buffon, Caceres, Bonucci, Chiellini, Evra, Lichtsteiner, Vidal, Marchisio, Pereyra, Tevez, Morata.
Roma XI (4-3-3)
De Sanctis, Torosidis, Manolas, Mapou, Cholevas, Pjanic, De Rossi, Keita, Gervinho, Totti, Ljajic
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni